Idadi ya watumishi hewa katika Mkoa wa Arusha imeongezeka kutoka 270 waliogundulika awali hadi kufikia 350, huku Serikali ikipoteza zaidi ya Sh1 bilioni kuwalipa mishahara.
Kwa ufupi
Kubainika kwa watumishi hao kumekuja baada ya agizo lililotolewa na Mkuu wa mkoa huo, Felix Ntibenda kufanya ukaguzi wa marudio kwa wilaya za Karatu na Meru.

